Wednesday, 27 August 2014

CHANONGO, MAGURI WACHEKA NA NYAVU SIMBA IKIITWANGA MAFUNZO 2-0


Simba imeendeleza wimbi la ushindi kwa kuichapa Mafunzo kwa mabao 2-0 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini haoa.
Mabao ya Simba yote mawili yalipatikana katika kipindi cha pili, akianza Elius Maguri katika dakika ya 63.
Shuti lake lilimshinda kipa Khalid Mahadhi, na dakika ya 71, Haruna Chanongo akafunga bao la pili.
Kiungo mkabaji wa Simba, Pierre Kwizera raia wa Burundi alipata balaa baada ya kuumia katika mchezo huo.
Katika mechi iliyopita ya kirafiki, Simba ilishinda kwa mabao 2-1

No comments:

Post a Comment