Sunday, 27 July 2014

SIMBA SC NA AZAM AKADEMI KATIKA PICHA LEO KARUME

SIMBA SC NA AZAM AKADEMI KATIKA PICHA LEO KARUME

Kiungo wa Azam FC, Mudathir Yahya akichuana na kiungo wa Simba SC, Aziz katka mchezo wa Robo Fainali michuano ya Rollingston asubuhi ya leo Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Azam FC ilishinda kwa penalti 3-2 baada ya sare ya 0-0.
Mchezaji wa Azam FC, Sadallah Mohamed kulia akichuana na Aziz wa Simba
Mshambuliaji Jamal Mchaulu 'Balotelli' wa Azam FC akimiliki mpira mbele ya beki wa Simba SC,  Omar Hussein
Mchezaji wa Azam FC, Christopher Mshanga kulia akimtoka mchezaji wa Simba, Omar Hussein
Wachezaji wa kikosi cha kwanza cha Simba SC, Amisi Tambwe na Shaaban Kisiga walikuwepo Karume kushuhudia wadogo zao
Kiungo wa Azam FC, Malik Mussa kushoto akimtoka beki wa Simba SC, Mbaraka Yussuf
Mchezaji wa Azam FC, Adam Omar akimuacha chini mchezaji wa Simba 
Kocha Mkuu wa Azam FC, Mcameroon Joseph Marius Omog alikuwepo
Kocha Mkuu wa Simba SC, Mcroatia Zradvko Logarusic (katikati) alikuwepo

No comments:

Post a Comment